Monday, November 24, 2014

KIKUNDI CHA KATAA UNENE FAMILY (KUF) CHAADHIMISHA MWAKA MMOJA

Kundi linalojulikana kwa jina la Kataa Unene Family (KUF) linaloongozwa na mwanadada Angel Msangi limeadhimisha mwaka mmoja tangu kuanzishwa kwake na kujiwekea malengo ya kusaidia idadi kubwa zaidi ya wenye uhitaji wa afya bora kwa kula kwa afya na mazoezi.

Kundi hilo lenye wanachama 30 limeadhimisha mwaka kwa kufanya mazoezi ya pamoja ikiwa ni pamoja na Aerobics, Kuogelea na Kucheza dansi katika Gym ya Rio iliyopo jijini Dar es Salaam na baadae kupata chakula cha pamoja cha usiku.
KUF ina wanachama kutoka mikoa mbalimbali nchini Ujerumani, Marekani na Uingereza.
Akizungumza katika sherehe hiyo ya maadhimisho ya mwaka mmoja, kiongozi wa kundi hilo Angel Msangi amesema anafarijika kuona watu wanapungua na kuwa na miili na ngozi nzuri kwa kuzingatia ushauri wa wataalamu na kuwa na nia kutoka moyoni
Kula kwa afya na kufanya mazoezi.
 Badhi ya Wanakikundi cha KUF walipokutana pamoja.
 Kila mmoja akitafakari.
 Marafiki wakifurahi.
 Mpiga picha wetu Ester Ulaya nae akipata ukodak.
 Wanakikundi wakiwa katika picha ya pamoja kabla ya kuanza kufanya mazoezi. 
 KUF wakifanya mazoezi.
Ukodak.
 Zoezi la kuogelea likiendelea baada ya Aerobics.
 Chakula
Kiongozi wa KUF Angela Msangi akikabidhiwa zawadi na Agnes Byera kwa kazi nzuri anayofanya ya kulingoza kundi.

2 comments:

sam mbogo said...

Safi sana Da Ester, nakikundi chako/chenu. unajuwa mwanamke akifanya mazoezi anapendeza zaidi.Hongereni sana. I la na waumezenu nao muwashawishi wajiunge nanyi kwe nye mazoezi.
kaka s

Interestedtips said...

Asante sana kaka Sam, usemalo ni sahihi kabisaa...itabidi nao wajoin